UTENZI WA AJALI YA MELI

Inasikitisha na kutisha,
hata tukiififisha
kamwe haiwezi kwisha;
yarabi atupe motisha,
moto tuweze washa;
Tuli hatuwezi pisha,
Hata wakitutapisha;

Katu haya si maisha,
Bora yalotutamanisha;
Kwanini haya yasoisha,
Japo miongo yatupisha?

Si Juma wala Aisha,
Wote kiyoro haitoisha;
Kibaya isotosha, kipi
Kwa haya maisha?

Pole walo mnazi,
Masahibu si zizi;
Tukiamua ni wazi,
Kutushinda hayawezi,
Muhimu kuweka wazi!

Walituambia juzi,
Ajali hawatoenzi;
Ahadi kama juzi,
Ajali kama enzi;

Bukoba walituasi,
Tukajua wako nasi;
Nungwi tena hasi,
Tena hamtuasi?

Si nzuri hali,
Kilio kila pahali;
Ahadi bado kali,
Si bado hatuna hali?

Ah, wacha tulie,
Wetu tujalie;
Hata tutulie,
Pemba itulie!

Majaribu yapo,
Siye pia tuwepo;
Wakuu watukerapo,
Hasira iwepo!

DBW, Leo.