Nimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya kifo cha mwandishi maarufu, Ben Mtobwaama ‘Joram Kiango’. Taifa limepoteza kinara mwingine wa kutumia fasihi andishi kufichua masuala mazito yaliyoigubika jamii yetu. Hivi karibuni nilimwona gwiji Ben pale kwenye Mkahawa wa Vitabu wa Somaakipanga mikakati ya uandishi na uchapishaji.
Nilidhani huo ni mwendelezo wa kumwona mpiganaji huyu akiwa katika harakati za kutumia ‘mtutu wa kalamu’ kufichua uzandiki na ufisadi katika jamii. Lakini upeo wa mwanadamu una kikomo. Hivyo, sikujua kuwa hiyo ilikuwa mara ya pili na ya mwisho kumwona mwanaharakati huyo ambaye pia alijitosa katika fani ya uhariri wa gazeti la Heko na uchapishaji kupitia kampuni yake ya Heko Publishers.
Nawasihi tumpe mtunzi huyu‘Zawadi ya Ushindi’ kwa kusoma kwa undani vitabu vyake ili tutambue ni nini hasa amejaribu kutufunulia ‘Nyuma ya Mapazia’ ya jamii yetu iliyozingirwa na ‘Malaika wa Shetani’ na mafisadi wenye ‘Roho ya Paka’ wanaomsulubisha ‘Mhariri Msalabani’ na kudiriki kusema ‘Najisikia Kuua Tena’ kupitia mikataba mibovu wanayoisaini ‘Dar-es-Salaam Usiku’ pasipo kumwambia mwekezaji uchwara ‘Peza Zako Zinanuka’ na tena bila kuogopa ‘Salamu Kutoka Kuzimu’ au kilio chetu cha ‘Tutarudi na Roho Zetu?‘ Buriani Ben Mtobwa!
Kweli hizi ni habari za kusikitisha sana. Bw. Mtobwa alikuwa mwandishi mahiri sana wa riwaya. Nakumbuka riwaya yake ya Dar es Salaam Usiku ilinifanya nichelewe kwenda shule wakati niko shule ya msingi nikaishia kuchapwa viboko. Mbali ya kwamba nilikuwa shule ya msingi, lakini nilitafuat hela na kuweza kununua riwaya zake nyingine kama Salamu kutoka Kuzimu na Pesa zako zinanuka.
Ni vizuri kumuenzi kwa kuendeleza yale mema aliyoyaacha.
Salaam zangu za pole ziwafikie Familia ya Ben Mtobwa na Watanzania kwa ujumlaa kupotelewa na mpiganaji mwanafasihi maridhawa Ben Mtobwa. Bwana ametoa na Bwana ametwa jina la Bwana libarikiwe.
Riwaya za Ben R. Mtobwa, Zilikuza sana Fikra zangu wakati ningali shule ya msingi. Zilinijenga sana kiakili na kifasihi, nikaishia kuwa Kijana mwenye Upeo sana katika Umri ule. Nimenunua upya vitabu vyake vyote kwa Ajiri ya wanangu ambao Tayari wameanza kuwa mahiri sana katika usomaji.
Oh Leo Ni Siku ya kuzaliwa Mwanangu, Ivyo nikasema nitatafuta simulizi za kusisimua Za Harakati za Joramu Kiango nianze kusoma kwa Upya lakn.Arusha nzima Nimekosa kwenye Maktaba zote za Mji.Niaingia mtandaoni kujaribu hata nisome online lakn Nimekutana na hizi taarifa shtuzi kuwa huyu nguri ni Marehemu,Mungu amlaze mahali pema peponi amen.Pia Kwa Anaeweza kunisaidia nipate Vitabu Vya Harakati Za Joramu Jaman anitafute kwa No zangub0764933857 Niko Arusha.