Chanzo cha matatizo yetu ni kuwa na vitu 2 tu kati ya vitu hivi 4 tunavyohitaji tuendelee kama vilivyoaInishwa na Mwalimu Nyerere:

1. Watu

2. Ardhi

3. Siasa Safi

4. Uongozi Bora

Suluhisho mmojawapo la matatizo yetu ni kuhakikisha kuwa hatuvipotezi na hivyo 2 tulivyo navyo maana tayari nguvukazi inapungua kwa sababu tunapoteza watu kupitia maradhi sugu, ajali holela na kadhalika. Na pia tunapoteza ardhi kupitia uwekezaji uchwara na uporaji. Utafiti wa Bajeti ya Kaya wa hivi karibuni unaonesha jinsi gani familia zetu zinavyoathiriwa na upungufu wa chachu kuu za maendeleo.

Lakini hilo suluhisho mmojawapohaliwezi kupatikana bila kutatua tatizo la ukosefu wa hivyo vitu vingine 2 vilivyobakia, yaani siasa safi na uongozi bora maana hivi tukiwa navyo ndipo tutaweza kudhibiti upotevu wa watu na ardhi. Na kamwe hatuwezi kuwa na utawala bora bila kuwa na uongozi bora. Hivyo, tuiangalie upya siasa yetu ya uongozi na mfumo wetu wa utawala.