Hivi ndivyo hali ya ujenzi wa barabara ya ‘central’ ilivyokuwa inaendelea mwishoni mwaka 2007 nikiwa safarini Kigali. Hali hii ilinikumbusha ahadi kedekede zilizotolewa na JK wakati wa kampeni za uchaguzi wa urais mwaka 2005. Baadhi ya ahadi hizo, kama hiyo hapo chini, zinapatikana hapa: http://www.hakielimu.org/Government_Promies.pdf

“I will make sure that the project to link Mtwara and Mwanza with a tarmac road is completed by December next year. Rich people driving saloon cars would be able to drive from Mtwara to Mwanza on a smooth road [Tafsiri: Nitahakikisha kuwa mradi wa kujenga barabara ya lami itakayounganisha Mtwara na Mwanza inakamilika Disemba mwaka ujao. Matajiri watakaokuwa wanaendesha magari madogo wataweza kuendesha kutoka Mtwara mpaka Mwanza kwenye barabara nzuri]” – JK