Na Jasper “Kido” (@KidoJapa)
Nani asiyependa mawingu kuyakata?
Nani mabawa akipata angani hatoruka? Ni wivu bila shaka na kijiba cha ukata, Mawaa yamewajaa Wasokheri washupaa, Nao ‘tasema kutwa wakichoka wataacha,
Wakorome kama chura
nami tembo sitoufyata, Nayo maji nitakunywa na sitojali vibaraka, Mchanga n’nalamba Kwa Jamhuri naapa, Magharibi nitakwenda Mashariki kadhalika, Kusi, kasi nitafika Baraka kuzichota,Ya wahenga yashapita
Hizi ni mpya kurasa, Zama kale si sasa Mambo yapaswa badilika, Kweli kizuri chajiuza Ila chapaswa pia jitembeza, Wala si Singida au Kilosa Bali Saudia na Ibiza, Katikati ya chochoro za Ulaya na Amerika Huko ndipo yapaswa katiza, Ziso haya ingia toka Ndizo watakazo zikumbuka,Achaneni na wanaobeza
Hawayajui ya wakubwa, Lini walishika madaraka Ndio waweze kutufunza, Tuwachunge yatupasa Hawana nia ya dhati kwa hakika, Tena tunapaswa jiuliza… Ipi dhamira yao, nchi yetu ‘kibaki nyuma? Ni vipi wao wataweza faidika? Ni kipi haswa wa’tuficha? Si watu wema hawa Ni wabaya na wanyama bila shaka,Watafura na kusema
na matusi kunivika, Hata nyimbo watatunga na makala kuandika, Sitojali, matope ‘kinipaka Wangu Mola atalipa, Ooh Ya Rabi Jalia Tiketi ninapokwenda kuikata, Uwe Rubani muongoza njia Niendapo kuyasaka mapesa, Kituo kinachofuata… ni kwenye visima vya mafuta.Comments are closed.
Kaka Kido. Hongera sana kiswahili kimetulia sana. Maelezo yamenyooka
Shukrani sana Kaka.
Ni shairi nzuri sana, limenipa hisia za kimapinduzi
Hongera mwanaharakati
Asante sana. Nimefarijika kusikia limeibua hisia njema kwako.
Wow…great!!
:)
Shairi zuri sana nimelipenda, nikama mshairi amechukua mawazo yangu yakila siku na kuwasilisha kwa ushairi mnono.
Erick, nimefarijika sana kuwa nimeweza kushughulika na kiu yako na kuweza kuyaweka mawazo yako katika kazi hii. Asante sana.
🦍
nzuri sana
Asante sana