Na Jasper “Kido” (@KidoJapa)

Nani asiyependa mawingu kuyakata?Nani mabawa akipataangani hatoruka?Ni wivu bila shaka na kijiba cha ukata,Mawaa yamewajaaWasokheri washupaa,Nao ‘tasema kutwawakichoka wataacha,

Wakorome kama churanami tembo sitoufyata,Nayo maji nitakunywana sitojali vibaraka,Mchanga n’nalambaKwa Jamhuri naapa,Magharibi nitakwendaMashariki kadhalika,Kusi, kasi nitafikaBaraka kuzichota,

Ya wahenga yashapitaHizi ni mpya kurasa,Zama kale si sasaMambo yapaswa badilika,Kweli kizuri chajiuzaIla chapaswa pia jitembeza,Wala si Singida au KilosaBali Saudia na Ibiza,Katikati ya chochoro za Ulaya na AmerikaHuko ndipo yapaswa katiza,Ziso haya ingia tokaNdizo watakazo zikumbuka,

Achaneni na wanaobezaHawayajui ya wakubwa,Lini walishika madarakaNdio waweze kutufunza,Tuwachunge yatupasaHawana nia ya dhati kwa hakika,Tena tunapaswa jiuliza…Ipi dhamira yao, nchi yetu ‘kibaki nyuma?Ni vipi wao wataweza faidika?Ni kipi haswa wa’tuficha?Si watu wema hawaNi wabaya na wanyama bila shaka,

Watafura na kusemana matusi kunivika,Hata nyimbo watatungana makala kuandika,Sitojali, matope ‘kinipakaWangu Mola atalipa,Ooh Ya Rabi JaliaTiketi ninapokwenda kuikata,Uwe Rubani muongoza njiaNiendapo kuyasaka mapesa,Kituo kinachofuata…ni kwenye visima vya mafuta.

  1. Capher June 14, 2022 at 10:34 am

    Kaka Kido. Hongera sana kiswahili kimetulia sana. Maelezo yamenyooka

    • Jasper Kido June 21, 2022 at 1:54 pm

      Shukrani sana Kaka.

  2. MODIMO MENDOZA June 14, 2022 at 10:37 am

    Ni shairi nzuri sana, limenipa hisia za kimapinduzi
    Hongera mwanaharakati

    • Jasper Kido June 21, 2022 at 1:55 pm

      Asante sana. Nimefarijika kusikia limeibua hisia njema kwako.

  3. Timothy June 14, 2022 at 11:37 am

    Wow…great!!

    • Jasper Kido June 21, 2022 at 1:56 pm

      :)

  4. Erick Ladslaus June 14, 2022 at 11:43 am

    Shairi zuri sana nimelipenda, nikama mshairi amechukua mawazo yangu yakila siku na kuwasilisha kwa ushairi mnono.

    • Jasper Kido June 21, 2022 at 1:57 pm

      Erick, nimefarijika sana kuwa nimeweza kushughulika na kiu yako na kuweza kuyaweka mawazo yako katika kazi hii. Asante sana.

  5. Eliona June 14, 2022 at 1:57 pm

    🦍

  6. Gladness S jackson June 14, 2022 at 2:11 pm

    nzuri sana

    • Jasper Kido June 21, 2022 at 1:56 pm

      Asante sana

Comments are closed.