HUYO NDIYE HAROUB

Profu Profesa nakwita, kimya shii umeshata

Wapi tutampata, wa namnayo kwa chapa?

Komredi twatafuta, mwenzetu wapi kapita?

Haroub wa Othman, utakumbukwa daima

Maendeleo na sheria, elimu lijipatia

Siasa, demokrasia, huko kote lipitia

Vitivo vingi liingia, taluma ajazilia

Usomi hiki na kile, katu sio kile kile

Haki lipigania, wanyonge wanamjua

Demokrasia lililia, Afrika inatambua

Usafi lilipalilia, ubaya liutumbua

Usomi sio maskuli, ni kutenda vile vile

Usomi si pesambele, usomi huduma mbele

Usome si kile kile, usomi hiki na kile

Ndio maltiprofeshenale, msomi namna ile

Lipokuwepo Harubu, liyafanya yote hayo

Usomi jamiitaa, uvunguni sio pake

Mkandala shule paa, nyumba enda uezeke

Jamii ipe kupaa, wanyonge na wainuke

Angekuwepo Harubu, nahaya angeyasema

Usije kuone tope, msomi ulikalie

Usije kuziba kope, motoni waungulie

Sije geuka upande, haki zao chukuliwe

Angetoa kawosia, nahaya angeyaamba

Huyo ndiye Harubu mapumzikoni

Haji hasauhuliki vitabuni

Nauliza nyi wasomi wa nchini

Mwafanyani mkumbukwe Tanzaniani?

Usomi pesambele na makelele?

Wasomi waibia wala matembele?

Uige vyake Harubu vipaumbele

Yani huduma mbele na utu mbele

© Immaculate Dominic