Na Abdilatif Abdalla
Nami nambe, niwe kama waambao
Niupambe, upendeze wasomao
Niufumbe, wafumbuwe wawezao

Kuna mamba, mtoni metakabari
Ajigamba, na kujiona hodari
Yuwaamba, kwamba ‘taishi dahari
 
Memughuri, ghururi za kipumbavu
Afikiri, hataishiwa na nguvu
Takaburi, hakika ni maangavu
 
Akumbuke, siku yake ikifika
Roho yake, ajuwe itamtoka
Nguvu zake, kikomoche zitafika
 
Afahamu, mtu hajuwi la kesho
Hatadumu, angatumiya vitisho
Maadamu, lenye mwanzo lina mwisho
 ———————————————-
*Shairi limechapishwa kwa idhini ya Abdilatif Abdalla
**Katuni imetumikwa kwa idhini ya Masoud Kipanya
  1. Ezekiel Kamwaga June 9, 2021 at 10:33 pm

    Yote I walaza chali, ina ghururi dunia. Ahsante Abdulatif

  2. Mfoi June 10, 2021 at 9:46 am

    Duh! Huyu mamba hatari!!

  3. Nassoro Abasi June 10, 2021 at 3:46 pm

    Nguvu ya Mamba ku’ mai

  4. Radiance Noordin June 11, 2021 at 12:17 pm

    Mamba anenwae hapa ni yupi?

  5. Hamza Rijal July 20, 2021 at 7:18 am

    Tuelezwe au aulizwe malenga Abdulateef Abdalla huyo mamba ni nani? Kwani hapa Taswira iliopo ni mtu ila kafafanishwa na Mamba, suala huyu Mamba ni nani? Naomba nifumbuliwe Kitandawili.

Comments are closed.