Jipu Hilo Jipu Gani?
Jipu Hilo jipu gani
Jipu lisilo na haiba
Jipu lisilo utani
Wala homa nasaba
Jipu liko ndani
Sistimu hukuna uhaba
Jipu limejaa uvundo usoni
Jipu lazima litumbuliwe
Bara na pwani
Mashariki kusini
Magharibi kaskazini
Mtumbuaji ashike pini
Huruma asiweke moyoni
Apasue jipu pwaaaa
Usaha uondoe nukhsani
Taifa letu adhimu
Lifurahie neema ya Mola mwenye Imani
Alotupa dhahabu na madini
Mito, mabonde, na mengi milimani
Hala Hala Watanzania,
Shangilia awamu yenye nidhamu
© Leila Sheikh
Can we Change?
By NeyK
Can we change 2015 to 61, to 64
Once more become independent, united,
A country we once were,
The people that once cared
About the green, yellow, black and blue on our flag (more…)
Wanafunzi wa Mwalimu Nyerere
Na Ado Shaibu (@AdoShaibu)
Moja tisa sita saba, kawakusanya Arusha
Wa taifa yeye baba, Azimio kufundisha
Wanafunzi kwa mahaba, wakajibu kwa bashasha
Zidumu fikira zako, hiyo ndo’ kauli yao
On The African Student
By Nephat Maritim
I have often wondered
Whether I should concede my identity to the mores of
the Ivory Tower
Whether I should let the snob define who I am, (more…)
Amina Chifupa – A Dream Deferred ?
Hers was a mission – a revolutionary mission
Hers was a dream – a liberating dream
Each generation, said Fanon, must discover its mission
Amina had discovered a mission (more…)
ATCL KULIKONI TWIGA WETU?
Wakati tunamshukuru Mungu kwa kuwanusuru abiria waliokuwa wamepanda ndege ya ATCL iliyopata ajali Kigoma na kusikitika kuhusu hali mbaya ya kampuni/shirika hilo huu ni wasaa wa kuirejea mistari hii ya shairi la Issa Bin Mariam almaarufu kamaProfesa Issa G. Shivji na kujiuliza, je, kulikoni kurejea kwa twiga wetu?
Twiga Katoroka – Kajiheshimu
Nimemkosa,
Sikumuona.
Akisimama wima,
Kama askari,
Na kiburi chake.
Kwa heshima na taadhima,
Akiimba kwa sauti nyororo:
“Mabibi na Mabwana,
Nawakaribisha kwenye
ndege hii ya Serengeti,
ndege ya Shirika la Ndege la Taifa.”
Twiga kakimbia,
Kenda kwao.
Kwao upo?
Mahali pake mkiani
Peupeeeeee….!
Nyeupe ya rangi,
rangi ya ubaguzi.
Ninashindwa,
kumeza.
Mkate na mayai, yao:
Prepared and Packed
in Pretoria.
Nimeinamisha kichwa.
Ninatetemeka kwa aibu.
Nawaona kwa kuibia.
Dada zangu wawili,
Wanyonge.
Bila tashi wala tamaa.
“Here we’re
Carlesberg for you, sir.”
“na…na….naomba safari.”
“I…I…I’d like safari.”
“Sorry…er….”
Twiga katoroka,
Kenda na heshima zake.
(Kajiheshimu)
Katorokea wapi?
Mbuga zao,
Watalii wao,
Ndege yao.
Kibendera chetu!
“Jjambo!
Captain Roaming Rogue speaking.”
Buriani Twiga.
Kwaheri za kuonana.
Kama sio kesho,
Keshokutwa.
3 Aprili 2003

