Poems2021-05-29T19:00:14+03:00

Jipu Hilo Jipu Gani?

Jipu Hilo jipu gani

Jipu lisilo na haiba

Jipu lisilo utani

Wala homa nasaba

Jipu liko ndani

Sistimu hukuna uhaba

Jipu limejaa uvundo usoni

Jipu lazima litumbuliwe

Bara na pwani

Mashariki kusini

Magharibi kaskazini

Mtumbuaji ashike pini

Huruma asiweke moyoni

Apasue jipu pwaaaa

Usaha uondoe nukhsani

Taifa letu adhimu

Lifurahie neema ya Mola mwenye Imani

Alotupa dhahabu na madini

Mito, mabonde, na mengi milimani

Hala Hala Watanzania, 

Shangilia awamu yenye nidhamu

© Leila Sheikh

Can we Change?

By NeyK

Can we change 2015 to 61, to 64
Once more become independent, united,
A country we once were,
The people that once cared
About the green, yellow, black and blue on our flag (more…)

On The African Student

By Nephat Maritim

I have often wondered

Whether I should concede my identity to the mores of
the Ivory Tower

Whether I should let the snob define who I am, (more…)

ATCL KULIKONI TWIGA WETU?

Wakati tunamshukuru Mungu kwa kuwanusuru abiria waliokuwa wamepanda ndege ya ATCL iliyopata ajali Kigoma na kusikitika kuhusu hali mbaya ya kampuni/shirika hilo huu ni wasaa wa kuirejea mistari hii ya shairi la Issa Bin Mariam almaarufu kamaProfesa Issa G. Shivji na kujiuliza, je, kulikoni kurejea kwa twiga wetu?

Twiga Katoroka – Kajiheshimu

Nimemkosa,

Sikumuona.

Akisimama wima,

Kama askari,

Na kiburi chake.

Kwa heshima na taadhima,

Akiimba kwa sauti nyororo:

“Mabibi na Mabwana,

Nawakaribisha kwenye

ndege hii ya Serengeti,

ndege ya Shirika la Ndege la Taifa.”

Twiga kakimbia,

Kenda kwao.

Kwao upo?

Mahali pake mkiani

Peupeeeeee….!

Nyeupe ya rangi,

rangi ya ubaguzi.

Ninashindwa,

kumeza.

Mkate na mayai, yao:

Prepared and Packed

in Pretoria.

Nimeinamisha kichwa.

Ninatetemeka kwa aibu.

Nawaona kwa kuibia.

Dada zangu wawili,

Wanyonge.

Bila tashi wala tamaa.

“Here we’re

Carlesberg for you, sir.”

“na…na….naomba safari.”

“I…I…I’d like safari.”

“Sorry…er….”

Twiga katoroka,

Kenda na heshima zake.

(Kajiheshimu)

Katorokea wapi?

Mbuga zao,

Watalii wao,

Ndege yao.

Kibendera chetu!

“Jjambo!

Captain Roaming Rogue speaking.”

Buriani Twiga.

Kwaheri za kuonana.

Kama sio kesho,

Keshokutwa.

3 Aprili 2003

Go to Top