Katika muktadha wa lugha nchini Tanzania, mtu anaposema ‘feki’ kwa Kiswahili, je, anamaanisha ‘fake’ kwa Kiingereza? Kwa mfano, wanafunzi wanaotafuta ‘mafeki’ kabla ya mitihani ya moko na ya taifa na kufanikiwa kuipata, je, wanamaanisha kuwa ni ‘fake’ kweli? Au wanamaanisha ni ‘kopi’ ya ‘orijino’ ama sehemu ya ‘orijino’?Ukiangalia na kusikiliza kwa makini maelezo katika kideo hicho hapo juu utaona kuwa kuna mstari mwembamba sana kati ya matumizi ya neno ‘feki’ na ‘orijino’. Pengine wanatumia lugha ya wanafunzi wanaosema ‘mafeki’ wakimaanisha ‘feki orijino’. Kama hivyo ndivyo, ina maana ‘feki’ lililosambazwa magazetini na mitandaoni ni dondoo tu ya kile kilichopo kwenye ‘orijino’?